IQNA

Uturuki yawakamata majasusi wa utawala wa Israel

10:44 - November 18, 2021
Habari ID: 3474572
TEHRAN (IQNA)- Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki amesema wanandoa wawili raia wa utawala haramu wa Israel waliokamatwa nchini humo wiki iliyopita walikuwa wanatekeleza ujasusi wa kijeshi na kisiasa.

Mume na mke walitiwa mbaroni na polisi ya Uturuki baada ya kupatikana wakipiga picha Ikulu ya Rais mjini Istanbul kinyume cha sheria.

Suleima Soylu amesema picha walizopiga jengo hilo hazikuwa zile za kawaida za kitalii bali zilionekana kuwa na ustadi wa juu kwa ajili ya kazi za kijasusi.

Amesema mwendesha mashtaka anaamini kuwa raia hao wa Israel walikuwa wanatekeleza ujasisi na sasa kesi yao itafikishwa mahakamani.

Soylu ni afisa kwa kwanza wa Uturuki kutoa taarifa rasmi baada ya kukamatwa Waisraeli hao wawili Jumatatu.  Uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwa walipiga picha hizo wakiwa katika mghahawa ulio katika eneo la juu la Mnara wa Mawasiliano wa Camlica Tower ambapo walizituma Israel kupitia WhatsApp huku wakiweka maelezo ya kitaalamu ya picha hizo.

Aidha walituma maelezo kuhusu idadi ya walinzi na taarifa zingine za siru za  Mnara wa Mawasiliano wa Camlica, ambao ni mnara mrefu zaidi wa mawasiliano bara Ulaya.

3476537

Kishikizo: israel uturuki jasusi
captcha