IQNA

Jaji Mwanamke Mmarekani Mwafrika ala kiapo kwa Qur'ani

15:30 - December 14, 2015
Habari ID: 3463116
Mwanamke Marekani Muislamu mwenye asili ya Afrika ameapishwa kwa kutumia Qurani kuwa jaji, katika jimbo la Brooklyn.

Carolyn Walker-Diallo ameapishwa kuwa jaji katika mahakama moja ya Wilaya ya Manispaa ya 7, katika jimbo la Brooklyn, baada ya kuteuliwa mwezi uliopita.
Diallo anakuwa mwanamke wa kwanza mwenye asili ya Afrika kuapishwa kuwa jaji nchini Marekani kwa kutumia Qurani.
Itakumbukwa kuwa, mwanamke wa kwanza Muislamu kuapishwa kuwa jaji nchini Marekani alikuwa Sheila Abdu-Salaam, katika mahakama ya juu ya New York, mwaka 1992.
Mwanamke mwingine Muislamu mwenye asili ya Kiarabu, Chalene Mekled Elder, aliajiriwa katika mahakama ya 3rd Circuit, jimboni Michigan mwaka 2006.
"Alhamdulillah, ni kwa unyeneyekvu mkubwa nakubali jukumu hili nzito kutoka kwa jamii yangu. Nitahakikisha kuwa kila mtu anapata uadilifu mahakamani," Walker ameandika katika tovuti yake.

3462831

captcha